Proverbs 6:1-5

Maonyo Dhidi Ya Upumbavu

1 aMwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako,
ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi
kwa ajili ya mwingine,
2kama umetegwa na ulichosema,
umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
3basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru,
kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako:
Nenda ukajinyenyekeshe kwake;
msihi jirani yako!
4 bUsiruhusu usingizi machoni pako,
usiruhusu kope zako zisinzie.
5 cJiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji,
kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
Copyright information for SwhNEN